Aliyeita mumewe ndovu apewa talaka India | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Tuesday, March 29, 2016

Aliyeita mumewe ndovu apewa talaka India

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Mahakama katika mji mkuu wa India imeamua kwamba ni kosa kwa mke kumuita mumewe “ndovu” na kosa hilo linaweza kuwa msingi wa talaka.
Mahakama Kuu mjini Delhi imedumisha uamuzi wa mahakama ya chini uliotolewa mwaka 2012 ambao uliidhinisha talaka.
Mahakama hiyo ilisema mtu kumuita mumewe ndovu ni “kumtendea ukatili wa kiakili”.
Mfanyabiashara aliyeitwa ndovu ana umri wa miaka 35 na alikuwa na uzani wa kilo 100.
Alisema mkewe alizoea kumuaibisha kwa kuwa mnene na "kutoweza kutimiza haja yake ya kimapenzi”, vyombo vya habari India vimeripoti.
"Hatua ya aliyekata rufaa kumbandika majina na kumrushia matusi mumewe kwa mfano kumuita 'Hathi' [ndovu], 'Mota Hathi' [ndovu mnene], hata kama alikuwa mnene bila shaka ingeathiri hadhi yake na kujiamini kwake,” Jaji Vipin Sanghi alinukuliwa na gazeti la India Today.
Mwanamke huyo alikuwa ameambia mahakama hiyo kwamba madai ya mumewe hayakuwa na msingi lakini mahakama haikukubaliana naye.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA