Erdogan aapa kukabili vikali magaidi | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Monday, March 14, 2016

Erdogan aapa kukabili vikali magaidi

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameapa kwamba atawakabili vikali magaidi baada ya shambulio la kigaidi kuua watu zaidi ya 36 mjini Ankara.
Bw Erdogan amesema shambulio hilo lililotekelezwa kupitia gari lililotegwa mabomu litazidisha kujitolea kwa maafisa wa usalama wa Uturuki.
Mlipuko huo ulitokea katika kituo muhimu cha uchukuzi cha Guven Park na kujeruhi zaidi ya watu 100. Mshambuliaji mmoja anadaiwa kuuawa.
Waziri wa mambo ya ndani Efkan Ala alisema uchunguzi utakamilishwa Jumatatu na kwamba wote waliohusika watatajwa.
Hakuna kundi lililokiri kuhusika lakini duru za serikali zinashuku chama kilichopigwa marufuku cha Kurdistan Workers Party (PKK).
    Twitter yapigwa faini na serikali Uturuki
    Rais amzuia mwanamume kujiua Uturuki
Waasi wa Kikurdi wametekeleza msururu wa mashambulio nchini Uturuki miezi ya karibuni na kuua mamia ya watu tangu kumalizika kwa mkataba wa kusitisha vita mwaka jana.
Kundi la Islamic State pia limetekeleza mashambulio Ankara karibuni.
Uturuki inashiriki katika mashambulio yanayotekelezwa na majeshi yanayoongozwa na Marekani dhidi ya IS na huruhusu ndege za kivita za muungano huo kutumia kambi yake ya ndege ya Incirlik kutekeleza mashambuli Iraq na Syria.
Pia imekuwa ikishambulia ngome za wapiganaji wa Kikurdi wa People's Protection Units (YPG) kutoka Syria, ambao imekuwa ikisema ni sehemu ya PKK.
Bw Erdogan kupitia taarifa amesema makundi ya kigaidi yanawalenga raia kwa sababu yanashindwa vitani na majeshi ya Uturuki.
Amehimiza kuwepo kwa umoja wa kitaifa lakini akasema Uturuki itatumia haki yake ya kujilinda kuzuia mashambulio siku zijazo.
"Watu wetu hawafai kuwa na wasiwasi, tutashinda vita hivi dhidi ya ugaidi na tutaangamiza ugaidi,” akasema.
Kwa mujibu wa shirika la habari la serikali nchini Uturuki, Waziri Mkuu Ahmet Davutoglu ameahirisha ziara yake ya Jordan kutokana na shambulio hilo.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA