Wazayuni: Tumeshindwa kuisambaratisha Intifadha ya Quds | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Thursday, March 10, 2016

Wazayuni: Tumeshindwa kuisambaratisha Intifadha ya Quds

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
Wazayuni: Tumeshindwa kuisambaratisha Intifadha ya Quds
Duru za Wazayuni zinaripoti kwamba, utawala ghasibu wa Israel umeshindwa kukabiliana na Intifadha ya Quds inayoendeshwa na wanamapambano wa Kipalestina.
Ripoti zinaeleza kuwa, katika mazingira ya hivi sasa Israel haina uwezo wa kukabiliana na wanamapambano wa Kipalestina na hivyo kuisimamisha Intifadha ya Quds iliyoanza Oktoba mwaka jana. Ron Huldai Meya wa Tel Aviv ameashiria woga na wahaka wa Wazayuni na kukosa amani kunakowakabili Wazayuni kutokana na kuendelea operesheni za wanamapambano wa Kipalestina na kubainisha kwamba, ukweli wa mambo ni kuwa, imekuwa haiwezekani kukabiliana na wanamapambano hao kwani wamekuwa wakitekeleza operesheni zao kwa kushtukiza.
Wakati huo huo, Ben Caspit mchambuzi mahiri wa Israel ameashiria jinsi mashirika ya usalama ya Israel yalivyochanganyikiwa katika kutoa majibu kwa operesheni za wanamapambano wa Kipalestina na kusema kuwa, mashirika hayo hayana uwezo wa kutoa mikakati ya kuhitimisha au hata kupunguza operesheni hizo za Wapalestina.
Mchambuzi huyo wa masuala ya kisiasa wa Israel ameyabeza na kuyaponda matamshi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na Yisrael Katz Waziri wa Usafiri na Barabara waliotaka kubaidishwa familia za watekelezaji wa operesheni za wanamapambano wa Kipalestina.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kuandamwa na kashfa mbalimbali za ufisadi na utovu wa maadili huku migogoro katika utawala huo ghasibu ikishadidi kila siku.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA