Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
China imeiwekea vikwazo vya kibiashara Korea Kaskazini ikitangaza marufuku ya kuingiza dhahabu na mkaa pamoja na kuliuzia taifa hilo mafuta ya ndege sambamba na masharti ya Umoja wa Mataifa.
Wizara ya biashara pia imepiga marufuku uingizaji wa vyuma adimu duniani vinavyotumiwa katika bidhaa za kiufundi.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lilipiga kura mwezi Machi ya kuongeza vikwazo hivyo dhidi ya Korea Kaskazini.
Uamuzi huo wa pamoja unajiri baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio jingine la silaha zake za kinyuklia mnamo mwezi Januari na kuzindua kombora jingine la masafa marefu mwezi uliofuatia.
Hatua hiyo inakaribia uidhinishaji wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa ambavyo China iliunga mkono.
Wengine wana wasiwasi kwamba Beijing haifuatilii vikwazo hivyo.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:
Post a Comment