Watano mbaroni kwa kujeruhi mwanafunzi | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Friday, May 6, 2016

Watano mbaroni kwa kujeruhi mwanafunzi

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
POLISI mkoani Kagera inawashikilia watu watano kwa tuhuma za kumjeruhi mwanafunzi Elizabeth Christian (17) wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Rumuli Manispaa ya Bukoba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi, alithibitisha kuwashikilia watu hao na alisema majina yao yanahifadhiwa kwa kuwa wanamtafuta Shaffy Rashid kwa tuhuma za kumtorosha mwanafunzi huyo.

Ollomi alisema kuwa Aprili 21 mwaka huu, mwanafunzi huyo alitoroka nyumbani kwao eneo la Nshambya na kuelekea kusikojulikana na kuwa baadaye iligundulika kuwa alitoroshwa na Rashid.

“Binti alitoroka kwao Nshambya na kuelekea eneo la Nyakanyasi, huko ndiko alikounguzwa kwa kumwagiwa maji ya moto,” alisema Kamanda Ollomi.

Binti huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, inadaiwa alimwagiwa maji ya moto na mwanamke aliyedai ana mahusiano na mumewe.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA