Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Jeshi la Marekani limesema kuwa limetekeleza shambulizi kwa kutumia ndege isiokuwa na rubani nchini Somalia, ikilenga gari moja lilokuwa limewabeba wanachama watatu wa kundi la kigaidi la al-Shabab.
Kulingana na msemaji wa pentagon, aliyelengwa hasa ni Hassan Ali Dhoore ambaye anatuhumiwa kuandaa mashambulizi ya hivi karibuni ya mabomu katika uwanja wa ndege wa Mogadishu na katika hoteli moja ambapo raia wa Marekani waliuwawa.
Shambulio hilo la majeshi ya Marekani limetekelezwa katika eneo la kaskazini mwa mji wa Jilib, karibu na mpaka wa Kenya na Somalia, huku Marekani ikisema ingali inatathmini matokeo ya shambulio hilo.
Shambulizi hilo la hivi karibuni la Marekani linajiri wiki chache baada ya shambulizi jingine katika kambi ya mazoezi ya al-Shabab kwa kutumia ndege zisizokuwa na rubani na nyingine iliokuwa na rubani.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:
Post a Comment