Apatikana na hatia ya kumuiba mtoto | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Thursday, March 10, 2016

Apatikana na hatia ya kumuiba mtoto

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Mahakama kuu mjini Cape Town nchini Afrika Kusini imempata na hatia mwanamke mmoja, kwa kumteka nyara mtoto mchanga kutoka hospitali moja karibu miaka 20 iliyopita.
Mtoto huyo anadaiwa kunyakuliwa kutoka kitanda cha mamake siku tatu baada ya kuzaliwa mnamo mwaka 1997.
Mwaka uliopita mtoto huyo aliunganishwa tena na familia yake baada ya kujenga urafiki na msichana mdogo katika shule yao ambaye walifanana sana.
Uchunguzi wa DNA ulithibitisha kuwa wasichana hao walikuwa ni dada wawili. Mwanamke anayeshutumiwa amekanusha kuhusika akisema kuwa alipewa mtoto na mtu mwingine baada ya kupoteza mimba.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA