Mtu asiyejulikana adai ''kumdukua'' Trump | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Sunday, March 20, 2016

Mtu asiyejulikana adai ''kumdukua'' Trump

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
Image
ImageTrump
Wiki mbili zilizopita mtu ambaye hakutaja jina lake alitangaza vita dhidi ya mgombea aliyekifua mbele katika chama cha Republican Donald Trump.
Na sasa akaunti inayodai kuwakilisha kundi la mdukuzi huyo limetoa kile linasema ni habari binafsi za Trump pamoja na zile za faragha.
Udukuzi huo unashirikisha habari za siri ikiwemo nambari ya simu ya mgombea huyo pamoja na bima ya usalama na eneo analoishi,tarehe yake ya kuzaliwa na majina ya wazazi wake.
Tulijaribu kulikagua kundi hilo kwa kutafuta katika mtandao kwa saa moja.
Na hivi ndivyo tulivyobaini.
Kwamba tarehe ya kuzaliwa ya Donald Trump,wazazi wake,watoto,tarehe ya eneo la kuzaliwa iko katika mtandao wa Wikipedia.
Habari hiyo pia inashirikisha ukurasa wa Mar-a-lago ,Palm Beach mjini Florida ambayo ndio anwani ilioorodheshwa katika udukuzi huo.
Eneo anakoishi pia lilibainiwa na wadukuzi hao lakini makao yake pia yanapatikana wakati mtu anapoyasaka katika huduma ya ramani ya Google.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA