Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Baada ya klabu ya Chelsea ya Uingerezakumfukuza aliyekuwa kocha wa klabu hiyoJose Mourinho miezi kadhaa iliyopita na nafasi yake kuchukuliwa na kocha wa mudaGuus Hiddink, April 4 uongozi wa Chelseaumetangaza kocha wa kudumu atakayejiunga na klabu hiyo mwishoni mwa msimu.
Chelsea imetangaza kuingia mkataba wa miaka mitatu na kocha wa timu ya taifa yaItalia Antonio Conte, Chelsea imempa mkatabaConte ambaye atajiunga na timu hiyo baada ya michuano ya Euro 2016 kumalizika akiwa anaiongoza timu ya taifa ya Italia katika michuano hiyo.

Antonio Conte
“Klabu ya Chelsea na soka la Uingereza kwa ujumla unaangaliwa sana popote uendapo, mashabiki wa soka Uingereza wanamapenzi na soka kweli, natumaini nitafurahia mafanikio hapa kama ilivyokuwa Italia” >>> Antonio Conte
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Antonio Conte aliwahi kuichezea timu ya taifa ya Italiakuanzia mwaka 1994 hadi mwaka 2000, lakini amewahi kuvifundisha vilabu vya Juventus yaItalia kuanzia mwaka 2011-2014, Siena na timu ya taifa ya Italia kuanzia mwaka 2014 hadi 2016. Conte kwa sasa ana umri wa miaka 46.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment