Jangili sugu Lauawa kwa risasi MPANDA | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Friday, May 6, 2016

Jangili sugu Lauawa kwa risasi MPANDA

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
MKAZI wa kijiji cha Busongola wilayani Mpanda anayedaiwa kuwa jangili sugu, Harumkiza Joshua (28), ameuawa kwa kupigwa risasi katika majibizano ya risasi na polisi waliokuwa kwenye msako maalumu wa wahalifu.

Aidha katika msako huo, Polisi imewakamata wakazi wanne wa kijiji hicho kwa kosa la kumiliki bunduki aina ya SMG namba TX 5971-1996, risasi 86, magazini mbili na nyama inayodhaniwa kuwa ya kiboko kilogramu mbili kinyume cha sheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Damasi Nyanda, alithibitisha tukio hilo na kuwataja watu hao wanne kuwa ni Amos Maliyatabu, maarufu kama ‘Samandale’ (70) na mwanawe James Amos ‘Samandale’ (28), Leoben Kagoma ‘Karumanzil’ (25) na Kulwa Joseph maarufu kwa jina la ‘Daniel’ (27).

Kamanda Nyanda alisema msako huo ulifanyika hivi karibuni katika kijiji hicho na maeneo mengine ya mkoa mzima. Alisema magazini moja ina uwezo wa kubeba risasi 30 na nyingine risasi 45 kwa wakati mmoja.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA