Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Kiongozi wa muda mrefu wa Zimbabwe Robert Mugabe amejibu kwa mzaha swali kuhusu mrithi wake na kusema bado anaweza kurusha ngumi.
Rais Mugabe aliulizwa nani atakayemrithi wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa.
Kiongozi huyo ambaye amekuwa uongozini tangu 1980 ametimiza umri wa miaka 92.
"Mbona unamtaka mrithi?" alimwuliza aliyekuwa akimhoji.
“Unataka nikutwange ngumi uanguke chini ndipo uamini kwamba bado nina nguvu?”, gazeti la serikali ya Herald limemnukuu.
Bw Mugabe, alisema hatastaafu katikati mwa muhula wake wa sasa, ambao ulianza 2013.
Mbunge ashtakiwa kumtusi mke wa Mugabe
Sing'atuki ng'o:Mugabe
“Mbona nikubali kuendelea kuongoza iwapo nina maradhi au ninaugua au siwezi kuongoza?” aliuliza.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:
Post a Comment