Chumba cha maiti Tumbi chafungwa na serikali | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Friday, March 11, 2016

Chumba cha maiti Tumbi chafungwa na serikali

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Serikali imefunga kwa siku tatu Chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya rufani ya Tumbi Mkoani Pwani kutokana na hali mbaya ya chumba hicho ukiwamo ubovu wa majokofu na huduma isiyoridhisha.
Akizungumza mara baada ya kufanya ziara hiyo Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinisia, Wazee na Watoto Mhe. Khamis Kigwangala amesema amechukua uamuzi huo baada ya kupokea maelezo kutoka kwa msimamizi wa chumba hicho.
Naibu waziri amesema amekuta changamoto kadhaa katika chumba hicho ikiwemo ubovu huo wa Mjaokofu hali inayosababisha maiti kulazwa sakafuni, na kupelekea kuharibika na kutoa harufu kali.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kigwangala amemtaka Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Elimu Kibaha kuandika barua ndani ya msaa 24 ya kujieleza kwanini asifukuzwe kazi kutokana na kushindwa kutatua changamoto zinazoikabili hosptali teule ya Tumbi.
Naibu Waziri huyo amesema amebaini kuwa kuna tatizo la kiutawala hali inayosababisha utoaji wa huduma za kimatibabu kuwa wa kusuasua ikwamo kukosekana kwa maji,ubovu na uchakavu wa chumba cha upasuaji, ukosefu wa dawa na chupa za kuhifadhia damu.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA