Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Utawala nchini Marekani unakata rufaa kupinga uamuzi wa jaji wa kukosa kuamrisha kampuni ya Apple kuifungua simu ya mkononi katika kesi moja inayohusu madawa ya kelevya.
Wizara ya sheria inatumia sheria sawa na iliyotumia katika majaribio yake ya kwanza ya kuitaka Apple kuifungua simu ya mwanamgambo aliyetekeleza mauaji katika eneo la San Bernardino.
Serikali ilienda mahakamani baada ya jaji katika neo la Brooklyn kusema kuwa hakuwa na mamlaka ya kutoa amri kama hiyo.
Katika kesi hiyo, serikali ya Marekani inamtaka jaji kuamrisha Apple iifungue simu ya Jun Feng, ambaye alikiri kuhusika katika ulangusi wa madawa ya kulevya.
Inataka kutumia simu hiyo kuwanasa baadhi ya washirika wake.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:
Post a Comment