Ndege ya kivita ya UAE yatoweka Yemen | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Monday, March 14, 2016

Ndege ya kivita ya UAE yatoweka Yemen

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Umoja wa Milki za Kirabau umesema ndege yake ya moja ya kivita imetoweka ikitekeleza mashambulio dhidi ya waasi wa Houthi nchini Yemen.
Shirika la habari la serikali ya nchi hiyo, WAM, lilitangaza kutoweka kwa ndege hiyo bila kutoa maelezo zaidi.
UAE imekuwa ikishiriki katika mashambulio ya muungano wa mataifa yanayoongozwa na Saudi Arabia kutekeleza mashambulio ya angani kumuunga mkono Rais Abedrabbo Mansour Hadi tangu Machi 2015.
Watu 6,000 wameauawa kwenye mapigano nchini Yemen.
Hicho ndicho kisa cha kwanza cha kutoweka kwa ndege ya UAE kwenye mapigano hayo.
Maafisa bado hayajaeleza ndege iliyotoweka ni ya muundo gani na pia iwapo marubani walidhurika.
Jeshi la wanahewa la UAE hutumia ndege za kivita aina ya F-16 na Mirage 2000.
Desemba, ndege aina ya F-16 ya jeshi la Bahrain ilianguka Saudi Arabia kutokana na “hitilafu za kimitambo”, na mwezi Mei ndege ya kivita ya Morocco ilitunguliwa nchini Yemen.
Ndege hizo mbili zilikuwa zikishiriki mashambulio dhidi ya waasi wa Houthi.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA