Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
Moja ya vyanzo vikubwa vya mapato vya ligi yoyote ni mapato yanayotokana na pesa zinazolipwa na haki ya matangazo ya television.
Kama tunavyolipa pesa kulipa pesa kwenye ving’amuzi basi kuna channel ndefu hadi club za kwenye ligi husika zinapata pesa zao kwa kile kiasi unacholipa kuangalia.
Kwa upande wa Chinese Super League pesa zinazolipwa kwa club za ligi ya china zimepanda mara 20 ukilinganisha kwa mwaka 2015 hadi mwwaka 2016.
Mwaka 2015 msimu ulipoisha club zilikua zinapata $9 millioni kutoka kwa warusha matangazo. Mwaka huu vilabu vinapata kiasi cha $200 milions kwenye mkataba wa miaka 5.
Ligi inaendelea kupata umaarufu kwa kusajili majina makubwa duniani na uwekezaji mkubwa unaendelea kufanyika. Hivyo basi ndani ya miaka michache ijayo inategemewa kuongezeka sana.
Ligi ya China kwa hapa Tanzania inaonekana kupitia Startimes pekee. Kuna wachezaji wa Africa wapo kwenye ligi hii na wengine wanazidi kuongezeka.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment