Twitter yaadhimisha miaka 10 tangu kuanza kutumiwa | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Tuesday, March 22, 2016

Twitter yaadhimisha miaka 10 tangu kuanza kutumiwa

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Mtandao wa kijamii wa Twitter unaadhimishwa miaka kumi tangu kutumwa kwa ujumbe wa kwanza kabisa.
Ujumbe wa kwanza kwenye mtandao huo ulitumwa na mwanzishili mwenzawa Twitter, Jack Dorsey, akisema: "just setting up my twttr" (ndio tu naanda twttr yangu).
Tangu wakati huo, mtandao wa Twitter umekuwa maarufu sana duniani na kutumiwa sana na wanasiasa, wanaharakati na wanahabari.
Ulichangia sana katika wimbi la mageuzi katika mataifa yaKiarabu na vitambulisha mada vingi vimetumiwa kusisimua hisia za watu.
Mfano ni kitambulisha mada ya #jesuisparis baada ya mashambulio ya Paris mwezi Novemba ambapo watu 130 waliuawa.
Wachezaji na wasanii ndio sana huwa na wafuasi wengi zaidi katika Twitter.
Wakati wa kilele chake, kampuni ya Twitter ilikuwa na thamani ya dola 25 bilioni za Marekani.
Lakini thamani ya kampuni hiyo imekuwa ikishuka, na pia imeshutumiwa kutokana na inavyoshughulikia unyanyasaji mtandaoni.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA