YANGA WAKABIDHIWA RASMI MZIGO WA WAARABU WA AL AHLY WA MISRI | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Saturday, March 19, 2016

YANGA WAKABIDHIWA RASMI MZIGO WA WAARABU WA AL AHLY WA MISRI

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Al Ahly imeimaliza Libolo kwa mabao 2-0 katika mechi kali Waarabu hao wababe wa soka wakiwa nyumbani. Sasa ni Yanga dhidi ya Ahly.

Yanga imeitoa APR kwa mbinde kwa jumla ya mabao 3-2, sasa inakutana tena na Al Ahly waliowatoa katika michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa.

Katika mechi ya leo, Al Ahly ilianza kupata bao lake katika dakika ya 10 Sobhy likadumu hadi mapumziko na kipindi cha pili ikafunga bao la pili kupitia Antui aliyemaliza kazi katika dakika ya 83.

Wakati wanaitoa Yanga, Ahly walionekana kuwa wachovu, kwani walilazimika kuwang’oa Yanga kwa mbinde wakiwa chini ya Kocha Hans van der Pluijm.

Pluijm  aliingoza Yanga kuitwanga Ahly bao 1-0 jijini Dar es Salaam, iliposafiri hadi Alexandria, Yanga ikafungwa bao 1-0. Wakaingia kwenye mikwaju ya penalti, ikang’oka.


Mbuyu Twite na Said Bahanuzi ndiyo waliopoteza penalti kwenye Uwanja wa Jeshi wa jijini Alexandria.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA