RAIS MAGUFULI AKATAZA WAKURUGENZI KWENDA NA MASHANGINGI DODOMA...SASA KWENDA NA COASTER | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Friday, April 15, 2016

RAIS MAGUFULI AKATAZA WAKURUGENZI KWENDA NA MASHANGINGI DODOMA...SASA KWENDA NA COASTER

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
Rais John Pombe Magufuli ameagiza kuwa Wakurugenzi wote wa Wizara mbalimbali watakaohudhuria vikao vya kamati za bunge Mjini Dodoma, watasafiri kwa mabasi badala ya magari yao "mashangingi" ya serikali kama ilivyozoeleka.

Katika utaratibu huo mpya kila Wizara itakodi basi (Coaster) kwa ajili ya kusafirisha Wakurugenzi hao kwenda Dodoma kwenye vikao vya bunge ili kutoa msaada kwa wizara zao pale wanapohitajika kufanya hivyo. Rais amefikia maamuzi haya ktk jitihada za kupunguza gharama za mafuta na posho za madereva wa wakurugenzi wanaposafiri kuelekea Dodoma.

Hata hivyo Wakurugenzi hao hawazuiwi kusafiri kwa magari yao binafsi (personal) kwa kujilipia gharama zote wao wenyewe ikiwa watataka kufanya hivyo. Katika utaratibu huu mpya inamaanisha kuwa viongozi wa wizara watakaosafiri kwa "mashangingi" kuelekea Dodoma ni Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu mkuu tu.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA