Tesla kuzindua gari la kielektroniki la bei ya chini | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Friday, April 1, 2016

Tesla kuzindua gari la kielektroniki la bei ya chini

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Kampuni ya magari ya Tesla imezindua gari lake lililotarajiwa na wengi aina ya Model 3,likiwa ndilo gari lenye bei ya chini ikilinganishwa na magari mengine ya kampuni hiyo.
Bei ya gari hilo lenye viti vitano italifanya gari hilo kuwavutia wateja wapya na huenda likavutia wateja zaidi kwa magari mengine ya kielektroniki.
Mkurugenzi mkuu wa Elon Musk,amesema kuwa lengo lake ni kuzalisha magari 500,000 kwa mwaka.
Kampuni hiyo yenye makao yake mjini California inalihitaji gari hilo kujiimarisha iwapo inahitaji kusalia katika soko lenye ushindani mkubwa.
Magari ya kwanza yataanza kuuzwa mwaka 2017,na yataweza kuagizwa kutoka mataifa mengi,ikiwemo UK,Ireland,Brazil,India,China na Newzealand.
Yale ya kawaida yatauzwa kuanzia dola 35,000 na yana kasi ya hadi kilomita 346 kila linapochajiwa.
Tesla ilitengeza magari 50,580 mwaka jana.
Magari mengi ni ya S Saloon, ambalo limelipiku gari la kielektroniki la Nissan Loaf na kuwa gari la kielektroniki linalouza sana duniani.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA