Mahakama yamlipa Hulk Hogan $115m | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Saturday, March 19, 2016

Mahakama yamlipa Hulk Hogan $115m

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Jopo la waamuzi mjini Florida limempatia aliyekuwa nyota wa mchezo wa mieleka Hulk Hogan kitita cha dola milioni 115 kama malipo baada ya mtandao mmoja wa udaku Gawker kuchapisha kanda moja ya ngono ya mchezaji huyo ambaye amestaafu.
Mawakili wa Bwana Hogan walihoji kwamba mtandao huo wenye makao yake huko New York ulikiuka haki za faragha za Hogan na kwamba kanda hiyo ilikuwa haina habari mpya.
Kesi hiyo iliokuwa na makabiliano kati ya uhuru wa vyombo vya habari dhidi ya haki ya faragha ya mtu maarufu ilifuatiliwa kwa karibu.
Kanda hiyo ya video ilichapishwa mwaka 2012 baada ya Hogan kurekodiwa akifanya ngono na mke wa rafikiye.
Mawakili wa Gawker walihoji kwamba ijapokuwa jopo la waamuzi huenda ukavichukia vitendo vya mtandao huo,swala la uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu sana.
Wakili wa Bwana Hogan alisema kuwa Gawker haikuwasiliana naye wala mwanamke aliyekuwa katika kanda hiyo kabla ya kuichapisha.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA