Paka mwizi wa nguo za ndani za wanaume | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Tuesday, March 22, 2016

Paka mwizi wa nguo za ndani za wanaume

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Paka mmoja mwizi wakati wa usiku amekuwa akiiba soksi pamoja na nguo za ndani nchini New Zealand.
Katika kipindi cha miezi miwili, paka huyo mwenye umri wa miaka sita kwa jina Brigit kutoka mji wa Hamilton aliiba suruali za ndani 11 na zaidi ya soksi 50.
Mmiliki wake Sarah Nathan alichapisha tabia ya paka huyo isiyo ya kawaida katika mtandao wake wa facebook.
''Tabia hiyo sasa inazidi kuwa mbaya.Lazima kuna mtu ambaye anakosa vitu vyake'',alisema katika chapisho lake la ukursa wa facebook lililosambazwa mara 500.
Bi Nathan amesema kwamba tatizo lilianza alipogundua vipande kadhaa vya nguo za ndani katika nguo zake anapoziosha.
''Suruali hizo za ndani hazikuwa zetu,na siku moja Brigit aliingia katika chumba cha wageni akiwa amebeba soksi aliongezea'',akisema kuwa waathiriwa wa Brigit walikuwa majirani katika nyumba za ghorofa.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA