Gari la wagonjwa lilikataliwa kupokelewa- Lema | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Thursday, April 14, 2016

Gari la wagonjwa lilikataliwa kupokelewa- Lema

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema CHADEMA amekabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Mwivaro 'Ambulace' ambayo itakayosaidia wagonjwa katika eneo hilo ikiwa ni moja ya ahadi zake kwa wananchi.

Akizungumza na EATV Lema amesema gari hilo alilinunua tokea mwaka jana lakini alikuwa amelipaki kutokana na serikali kukataa kulipokea kwa hofu kwamba wangempa umaarufu wa kisiasa.

''Gari hili nililinunua mwaka jana lakini serikali wakakataa kulipokea nikalipaki na nikahimiza wananchi wa jimbo langu kunichagua ili tulete maendeleo ya kweli na baada ya kupata madiwani wa kutosha na Meya wa jiji sasa wananchi wategemee mambo makubwa zaidi katika jimbo langu na jiji kwa ujumla''-Amesisitiza Lema.

Aidha Mbunge huyo amesema kwa sasa anafanya kazi za maendeleo vizuri kwa kushirikiana na viongozi wa serikali na hakuna tatizo kubwa katika mahusiano ya viongozi wa serikali kama ilivyokuwa hapo awali.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA