Wanawake 2 vikongwe wameuawa kinyama wilayani Rorya mkoani Mara | MAUJANJA 24 NEWZ

HABARI ZA KITAIFA,KIMATAIFA,KUMBUKUMBU ZA KIHISTORIA,MICHEZO NA BURUDANI,NA MENGINE MENGI

Breaking News
Loading...

Thursday, April 14, 2016

Wanawake 2 vikongwe wameuawa kinyama wilayani Rorya mkoani Mara

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja
Wanawake wawilivikongwe wameuawa kinyama kwa kupigwa na kukatwakatwa kwa mapanga kisha miili yao kuchomwa moto katika kijijicha Kenyamsana wilayani Rorya mkoani Mara kwa tuhumu za kujihusisha na ushirikina,tukio ambalo limesababisha hofu kubwa kwa wanawake wengi wenye umri mkubwa katika kijiji hicho.

Wakizungumzia tukio hilo la kwanza kutokea wilayan Rorya, baadhi ya ndugu wa marehemu hao, wamesema kuwa kundi la watu waliwakamata wanawake hao vikongwe kisha kuwapiga katika sehemu mbalimbali za miili huku wakiwaingiza kwa nguvu ndani ya nyumba zao ambazo zimeezekwa kwa kutumia nyasi na kuwachoma moto.

Kufutia tukio hilo la kusikitisha na la kikatili Mwenyekitiwa kamati ya ulinzina usalma ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Rorya Bw Felix Lyaniva, amefika eneo la tukio na kuliagiza jeshi la polisi kuwakata watu wote ambao wamehusika kufanya kitendo hicho cha kinyama kwa kuanzia na viongozi wa vitongoji katika eneo hilo.

Tayari Jeshi la Polisi limewakamata watu 13 kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo ya wanawake hao vikongwe Bi Ghati Ndege na Nyakorema Waryuba wote wakazi wa k ijiji hicho cha Kenyamsana wilayani Rorya.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

google+

linkedin

Maujanja Yote Tz Blog
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0755-207374. Soma Zaidi

    0 comments:

     

    IDADI YA WASOMAJI

    TAFUTA HABARI HAPA