Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Kwa Kubonyeza Like Hapa Chini Nikutumie Habari Moja Kwa Moja

Kocha wa zamani wa klabu ya FC Barcelona yaHispania ambaye kwa sasa anaifundisha klabu ya FC Bayern Munich akimalizia mkataba wake, kabla ya kujiunga na Man City mwishoni mwa msimu Pepe Guardiola, tayari mechi yake ya kwanza akijiunga na Man City kuna tetesi kuwa imejulikana.
Pepe Guardiola anatajwa kuwa na tetesi mechi yake ya kwanza itakuwa dhidi ya Man Unitedambayo inadaiwa kuwa kwa wakati huo itakuwa ikifundishwa na Jose Mourinho, ila itakuwa ni michuano ya maandalizi ya msimu‘International Champions Cup’ itakayofanyikaBeijing China.

Kutoka kushoto ni Jose Mourinho na Pep Guardiola
Hata hivyo ukweli wa kukutana au kutokukutana utajulikana wiki hii, kwa sasa mashabiki wa Man United wanaimani kuwaLouis van Gaal atafukuzwa mwishoni mwa msimu na Mourinho atajiunga nao, wakati Man City wao walithibitisha kuwa tayari walisaini mkataba na Guardiola.
KUPATA HABARI NA MATUKIO YA KILA SIKU, BONYEZA Like HAPA CHINI
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment